Jana tuliendelea kuangazia mada hii mhimu. Tuligusia na kuangalia sababu za mwajiri kwa nini anataka mfanyakazi, tuliona ni kwa lengo tu la kutimiza malengo yake kwa kujiongezea mikono zaidi ya miwili aliyonayo.Leo tena tuangazie kipengele kingine, karibu
2. Unaajiriwa uli ulipwe mshahara.
Lengo la kila binadamu kuajiriwa hapa Duniani, ni ili alipwe mshahara akiwa na maono ya kukidhi mahitaji yake ya kila siku. Ajira humpatia mtu ridhiki yake ambayo hutokana na anacholipwa kutokana na kazi anayoifanya. Mwajiriwa huyu hupangiwa malipo atakayopokea kutoka kwa mwajiri wake, hivyo hana uhuru wa kupanga alipwe kiasi gani! Mwajiri ndiye hupanga akulipe kiasi gani. Ukishindwa kukubaliana na malipo anayokupa, basi unahiari ya kuacha kazi ukatafute sehemu nyingine, yeye hata hawezi kuumia kwa sababu anaamini ataajiri mtu mwingine na yamkini atamlipa kiasi kidogo zaidi ya alichokusudia kukulipa wewe. Na hii ni kwa sababu mwajiri anaamini wanaotafuta ajira ni wengi na maisha kwa wengi ni magumu, hivyo wako radhi kufanya kazi hata kwa malipo kidogo yanayoweza kukidhi mahitaji ya kula tu. Na mwajiriwa hupata mapato yake kila baada ya mwezi mzima jambo ambalo ni baya sana kwa usitawi wa maisha ya binadamu anayetaka kuendelea. Mwajiri yeye huingiza kipato kila siku kupitia mwajiriwa wake, wakati mwajiriwa huingiza kipato kila mwezi kutoka kwa mwajiri wake.
Mwajiri anakulipa kiasi tu kidogo sana kutoka kwenye faida anayoipata, hata kama ukilipwa kiasi kikubwa- basi ujue faida ya mwajiri wako ni kubwa zaidi, na anakulipa tu ili uendelee kumfanyia kazi zake. Na ndiyo maana faida yake ikipungua sana anapunguza wafanyakazi ili kukidhi matakwa yake ya kuingiza zaidi.
Tukutane wakati mwingine
Ni mimi mwezeshaji wako
Ngusa J.