Kila siku vyuo vinabuniwa, kuanzishwa, kusajiliwa, kudahili na kupokea wanafunzi. Wakati huo vyuo vingine kila mwaka vinaandaa na kufanya mahafali za kuwaaga wahitimu wao. Mfumo wetu wa Elimu unawalazimisha wahitumu hawa aidha kusubiria ajira za serikali au kuzunguka na bahasha maofisini ili wapate ajira. Wachache sana ambao husoma wakiwa na malengo ya kujiajiri. Hata wamalizapo chuo hupitia wakati mgumu sana kuzisaka ajira na hapo ndipo huja wazo la kujiajiri, lakini hawana mitaji-waanzie wapi? Lakini swali muhimu linakuja, KWA NINI UNAAJIRIWA?
Hapa ndipo tunaweza anza uchambuzi wa swali hili adimu. Jibu ni moja tu- Unaajiriwa ili ulipwe mshahara. hivyohivyo kinyume chake, unajiajiri ili ujilipe mshahara, unaajiri ili ulipe mshahara. Lakini mada yetu kwa sasa ni kwa nini unaajiliwa? Tukutane kesho kwa uchambuzi hapahapa mtandaoni.
Ni mimi mhamasishaji wako
Ngusa J.
+225757990751/+255625163596
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni