Jumanne, 20 Septemba 2016

TUHAMIENI KWENYE UJASIRIAMALI


Maisha mtaani yamezidi kuwa magumu kwa watu wengi. Kila mmoja anajaribu kujikomboa kivyake, wengine wanaungana, wengine wanatengana, wengine wanaanzisha biashara, wengine biashara zao zinakufa, wengine wana mitaji ila hawajui waiwekeze wapi? Wengine wanawazo la biashara (Bussines idea) lakini hawana mtaji na hawajui pa kuupata, wengine wanasubiri ajira za serikali, wengine wanatoka kwenye ajira za serikali wakilenga kujiajiri wenyewe, wengine wanaajiri, wengine wanafukuza wafanyakazi, wengine wanaendesha mikokoteni- Wote hawa lengo lao kuu ni moja tu, kupambana na umasikini. Lakini hebu tutafakari pamoja maswali haya matatu;

1.Kwa nini uajiliwe?
2.Kwa nini ujiajiri?
3.Kwa nini unaajiri?

Naamini maswali haya matatu ni muhimu sana kwa mtu yeyote aliyelenga kupambana na adui dhalimu umasikini. Team yetu imeamua kukufikia wewe mjasiriamali, unayetegemea kuwa mjasiriamali na unayewaza kutoka kwenye ujasiriamali. Tumeamua kukufikia kwa njia ya mtandao huu, tukushirikishe, utushirikishe pia. Tutakuletea mada nyingi sana zitakazokuzindua na kukufanya uweze kufikia malengo yako. Pia timu yetu itakuhudumia katika nyanja zote za ujasiriamali ikiwa ni pamoja na kukuandalia Business plan kwa ajili ya biashara yako. Stay tuned...
Ni mhamasishaji wako
Ngusa J.
+225757990751/+225625163596

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni